Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi amesema kuwa, hatasalimu amri
kwa wale wanaofanya njama kutaka asigombee urais katika uchaguzi mkuu
ujao nchini humo.
Hayo yamesemwa na Willy Nyamitwe, mshauri wa Rais Nkurunziza
akimnukuu rais huyo ambapo pia amekosoa maandamano ya wapinzani
wanaopinga azma yake ya kushiriki katika uchaguzi ujao na kuitaja hatua
hiyo kuwa ni kinyume na demokrasia. Nyamitwe amesisitiza kuwa, Rais
Nkurunziza hatasalimu amri katika azma yake hiyo. Amewataja wale
wanaoandamana kupinga hatua hiyo kuwa, wanatishia usalama wa wananchi
katika uchaguzi ujao.
Mshauri huyo wa raia wa Burundi anasema chama tawala CNDD-FDD, kama
vilivyo vyama vingine vya siasa na katika fremu ya mwenendo wa
kidemokrasia, kina haki ya kumteua mgombea yeyote kimtakaye.
Kwa muda wa siku tatu sasa, maeneo kadhaa ya Burundi yamekuwa
yamekumbwa na machafuko makali ambayo yamesababishwa na hatua ya chama
tawala CNDD-FDD kumuidhinisha Rais Nkurunziza kupeperusha bendera ya
chama hicho katika uchaguzi ujao
No comments:
Post a Comment