Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Saturday, 25 April 2015

Nkurunziza atangazwa rasmi kugombea urais Burundi

Chama tawala nchini Burundi cha CNDD-FDD leo kimemtangaza rasmi Rais Pierre Nkurunziza wa nchi hiyo kuwa ndiye atakayepeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi ujao wa Rais mwezi Juni mwaka huu. Akitangaza uamuzi huo katika mkutano wa CNDD-FDD uliofanyika leo mjini Bujumbura, mwenyekiti wa chama hicho Pascal Nyabenda amesema kama ninavyomnukuu: “Tuna furaha kuwatangazia wananchi wa Burundi na ulimwengu kwa ujumla kwamba, chama cha CNDD-FDD kimemteua Rais Nkurunziza kuwa mgombea wake katika uchaguzi ujao wa Rais”. Mwisho wa kunukuu. Mwenyekiti huyo wa chama tawala nchini Burundi amesema kuwa, wanawataka wapinzani wao kuwa watulivu na kwamba, wakachuane na Rais Nkurunziza katika masanduku ya kupigia kura. Aidha amesema, chama hicho kinavitaka vikosi vya usalama na polisi kuwachukulia hatua wale wote watakaojitokeza barabarani kupinga uamuzi huo. Wakati huo huo, vyama vya upinzani nchini Burundi vimeapa kwamba, vitasimama kupinga uamuzi huo ambao vimesema unakinzana wazi na katiba hasa kwa kutilia maanani kwamba, kiongozi huyo ameshaingoza nchi hiyo kwa duru mbili. Taarifa zaidi zinasema kuwa, uamuzi huo unaweza kuzusha machafuko katika nchi hiyo ambayo imeshuhudia amani na utulivu tangu mwaka 2005 baada ya kumalizika vita vya wenyewe kwa wenyewe

No comments:

Post a Comment