Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Tuesday, 28 April 2015

Al Bashir ashinda uchaguzi wa Rais Sudan

Kamisheni Kuu ya Uchaguzi nchini Sudan imetangaza kuwa Rais wa sasa wa nchi hiyo Omar al Bashir ameshinda tena kiti cha rais kwa kupata asilimia 94 ya kura za uchaguzi uliofanyika mwezi huu.
Taarifa ya kamisheni hiyo pia imesema chama tawala cha Congresi ya Taifa kimeshinda uchaguzi wa Bunge kwa kupata viti 323 kati ya viti vyote 426. Mkuu wa Kamisheni ya Uchaguzi ya Sudan, Mokhtar al-Assam amesema asilimia 46.4 ya watu karibu milioni 13 waliojiandikisha ilishiriki katika zoezi hilo lililofanyika kwa siku nne kuanzia Aprili 13.
Al Bashir mwenye umri wa miaka 71 amepata kura milioni 5 lakini mbili elfu 52 na 478 kati ya kura zote sahihi milioni 5, 584 elfu na 863. Mpinzani wake wa karibu katika uchaguzi huo, Fadhl Assayyid Shuaib amepata asilimia 1.43 ya kura.
Al Bashir ambaye ameiongoza Sudan kwa kipindi cha miaka 25 anasakwa na Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kwa tuhuma za kutenda jinai za kivita katika jimbo la Darfur.

No comments:

Post a Comment