Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Saturday, 25 April 2015

Hizbullah: Uvamizi wa Saudia Yemen utashindwa tu

Naibu Katibu Mkuu wa harakati ya muqawama wa Kiislamu ya Lebanon Hizbullah amesema Saudi Arabia itashindwa tu katika uvamizi wake dhidi ya Yemen. Sheikh Naeem Qasim, ameongeza kuwa dunia leo inashuhudia kipigo cha kufedhehesha inachopata Saudi Arabia; na licha ya mashinikizo yote, harakati ya wananchi ya Ansarullah pamoja na jeshi la Yemen zinaendelea kudhibiti maeneo mengi ya kaskazini na kusini mwa nchi hiyo. Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah amesisitiza kuwa kadiri vita vikichukua muda mrefu zaidi ndivyo kushindwa kwa Saudia kutavyozidi kudhihirika. Katika upande mwengine ripoti kutoka Yemen zinaeleza kuwa majeruhi walioko kwenye mkoa wa Sa’dah wako katika hali mbaya kutokana na kuzingirwa mkoa huo na kushindwa misaada ya tiba kuwafikia watu hao. Muhammad Hajr, Mkurugenzi Mkuu wa hospitali ya al Jamhuri mkoani Sa’dah amesema kuendelea mashambulio ya ndege za kivita za Saudi Arabia na kushindwa kufika misaada ya tiba kutokana na mzingiro kumezifanya hali za majeruhi katika mkoa huo ziwe mbaya zaidi. Akiashiria kuendelea mashambulio ya ndege za kivita za utawala wa Aal Saud dhidi ya taasisi muhimu na miundomsingi ya Yemen, Muhammad Hajr ameziomba jumuiya za kimataifa kufanya jitihada ili kuepusha kutokea maafa ya kibinadamu nchini humo. Wito huo umetolewa katika hali ambayo kwa mara nyengine tena ndege za kivita za Saudia jana zilizuia kuingia kwenye anga ya Yemen na kutua kwenye uwanja wa ndege wa Sana’a ndege ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iliyobeba misaada ya kibinadamu na shehena za madawa na vyakula.
Katika medani za mapambano, ripoti zinaeleza kuwa mkoa wa Ma’rib unadhibitiwa kikamilifu na harakati ya Ansarullah. Duru moja ya kijeshi ya Yemen imetangaza kuwa baada ya vikosi vya gadi ya Rais vyenye mfungamano na Rais wa zamani wa nchi hiyo Ali Abdullah Saleh kujiunga na harakati ya wananchi ya Ansarullah, mkoa wa Ma’rib ulioko katikati mwa nchi hiyo uko chini ya udhibiti kamili wa harakati hiyo ya wananchi…

No comments:

Post a Comment