Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Wednesday, 8 April 2015

Waislamu UK: Vijana wanahadaiwa kujiunga na Daesh

Kiongozi mmoja wa zamani wa mahakama nchini Uingereza amesema kuwa, vijana wengi wa nchi hiyo wamejiunga na kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh baada ya kurubuniwa. Nadhir Afdhal, mmoja wa viongozi wa Kiislamu aliyewahi kuhudumu katika vyombo vya mahakama nchini Uingereza amesema kuwa, mfumo wa kuwarubuni vijana unaotumiwa hii leo ndio chanzo cha vijana kuendelea kujiunga na magaidi. Amesisitiza kuwa, Uingereza na nchi nyingine za dunia zinatakiwa kuchukua hatua za kisasa katika kukabiliana na mfumo huo hatari unaowaingiza vijana wengine katika wimbi la ugaidi.
Kwa mujibu wa msomi huyo, magaidi wanatumia njia za kisasa katika kujitangaza, suala ambalo limewafanya vijana wengi waathiriwe na propaganda hizo. Hayo yamekuja wakati ambao hivi karibuni, ilitangazwa habari ya kutiwa mbaroni mtoto wa mwanaharakati mmoja wa chama cha Leba nchini Uingereza akiwa pamoja na Waingereza kadhaa waliokamatwa katika mpaka wa Uturuki wakielekea Syria kwa ajili ya kujiunga na makundi ya kigaidi yanayopigana na jeshi la serikali ya nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment