Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 27 April 2015

Wanne wauawa katika mashambulio ya Israel Golan

Watu wanne wameuawa katika mashambulio ya anga ya utawala wa Kizayuni wa Israel kwenye miinuko ya Golan inayokaliwa kwa mabavu na utawala huo, karibu na mpaka wa Syria. Wahanga wa mashambulio hayo ya Israel ya jana usiku yaliyotekelezwa karibu na mji wa Majdal Shas, bado hawajatambuliwa hadi sasa.  Israel imefanya shambulio hilo jana usiku kwenye miinuko ya  Golan,  siku mbili baada ya utawala huo kuzishambulia kambi za jeshi la Syria  huko katika eneo Qalamoun karibu na mpaka wa nchi hiyo na Lebanon. Miinuko ya Golan imekuwa ikikaliwa kwa mabavu na utawala wa Kizayuni wa Israel tangu muongo wa 60. Utawala wa Tel Aviv uliikalia kwa mabavu ardhi ya miinuko ya Golan yenye ukubwa wa kilomita 1200 wakati wa Vita vya Siku Sita mnamo mwaka 1967na kisha kulitwaa eneo hilo mwaka 1981

No comments:

Post a Comment