Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Sunday, 26 April 2015

AI yataka kupanuliwa oparesheni za kuokoa wahajiri

Shirika la Msamaha Duniani (Amnesty International) limetaka kupanuliwa oparesheni za kuwatafuta na kuwaokoa wahajiri wanaolekea barani Ulaya kutokana na kusafiri katika mazingira hatari katika bahari ya Mediterranean. Gauri van Gulik, Naibu Meneja wa shirika hilo la haki za binadamu barani Ulaya amesema kuwa operesheni za uokoaji zinapaswa kupanuliwa hadi kwenye maeneo ya karibu na pwani za Libya. Amesema wahajiri mara kwa mara wamekuwa wakitumia boti kuukuu ili kujaribu kufikia pwani za nchi za Ulaya na kwamba polisi wa doria wamekuwa wakikagua maeneo ya karibu na mipaka ya Italia pekee. Naibu Meneja wa Amnesty International barani Ulaya amesema hayo kufuatia ajali ya boti ya hivi karibuni katika bahari ya Mediterranean iliyouwa watu 800. Tarehe 16 mwezi huu msemaji wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) alithibitisha kuwa watu 800 walikufa maji kufuatia ajali ya boti katika bahari hiyo. Boti hiyo ilizama katika umbali wa kilomita 96 kutoka pwani ya Libya wakati ilipokuwa inaelekea Italia

No comments:

Post a Comment