Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Thursday, 23 April 2015

Kumshikilia Sheikh Salman si suluhisho kwa Bahrain"

Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kuongezwa muda wa kushikiliwa korokoroni Sheikh Ali Salman, Katibu Mkuu wa Harakati ya Kiislamu ya al-Wifaq ya Bahrain hakusaidii chochote katika kuyapatia ufumbuzi matatizo ya nchi hiyo. Marzieh Afkham amebainisha kwamba, kuendelea kutawala mazingira ya kipolisi nchini Bahrain kunaifanya hali ya mambo nchini humo izidi kuwa tata. Afkham amesisitiza kuwa, watawala wa Bahrain wanapaswa kuzingatia suala la mazungumzo na kuheshimu matakwa ya wananchi sambamba na serikali ya Manama kuchukua hatua zitakazoandaa mazingira ya kuweko hali ya kuaminiana. Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema bayana kwamba, kuheshimu matakwa ya wananchi ni jambo muhimu mno. Wakati huo huo, mwanazuoni mashuhuri nchini Bahrain Sheikh Issa Qassim amesema kuwa, kuendelea kutiwa mbaroni wanaharakati wa kisiasa ni ishara ya wazi kwamba, watawala wa Manama wameng’ang’ania kuendeleza siasa za ukandamizaji.

No comments:

Post a Comment