Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 1 May 2015

Mapigano mapya yaua watu 19 kaskazini mwa Mali

Watu wasiopungua 19 wameuawa katika mapigano yaliyozuka baina ya waasi wa Tuareg na wanajeshi wa serikali, kaskazini mwa Mali. Wizara ya Ulinzi ya Mali imetoa taarifa ikisema kuwa, wanajeshi 9 wameuawa baada ya waasi wa Tuareg wa CMA wanaopigania kujitenga eneo la Azawad kuushambulia mji wa Lere karibu na mpaka wa Mali na Mouritania siku ya Jumatano. Taarifa hiyo ya jana ya Wizara ya Ulinzi ya Mali imeongeza kuwa, wanajeshi wengine 6 wamejeruhiwa kwenye shambulio hilo na wengine sita kutekwa nyara. Wanajeshi wa Mali walifanikiwa kuua waasi 10 wa Tuareg na kuwajeruhiwa wengine 16 kwenye mapigano hayo. Vile vile walifanikiwa kuharibu magari ya waasi hao na kuteka silaha zao kadhaa. Wakati huo huo Waziri wa Ulinzi wa Mali Tieman Hubert Coulibaly amesema kuwa mji wa Mali bado umo mikononi wa serikali. Eneo la kaskazini mwa Mali limeshuhudia siku kadhaa za machafuko. Serikali ya Bamako inawalaumu waasi kwa kuchoche machafuko hayo ikisema kuwa waasi hao wamekusudia kuharibu kwa makusudi mwenendo wa mazungumzo ya amani nchini humo.

No comments:

Post a Comment