Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Tuesday, 21 April 2015

'Marekani ilianzisha kundi la kigaidi la Daesh 2006'

Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, kundi la kigaidi la Daesh lilianzishwa mwaka 2006 kwa usimamizi wa Wamarekani. Rais wa Syria amesisitiza kwamba, kundi hilo la kigaidi lilianzishwa na Marekani na kuongeza kuwa, muungano wa kimataifa unaoongozwa na Marekani kwa ajili ya kupambana na kundi hilo la kigaidi hadi sasa haujawa na nia ya dhati ya kuwatokomeza magaidi hao. Rais Assad ameikosoa Ufaransa na baadhi ya madola mengine ya magharibi kwa kuwaunga mkono wapinzani wa Syria na kusema bayana kwamba, kundi la kigaidi la Daesh lilianzishwa mwaka 2006 huko Iraq kwa usimamizi na uongozi wa Marekani. Aidha Rais Assad amekanusha vikali madai kwamba, jeshi la Syria limetumia mabomu ya kemikali katika mashambulio yake huko Idlib na kubainisha kwamba, Damascus haioni haja ya kufanya hivyo. Kuhusiana na ushirikiano wa Syria na Magharibi, Rais Bashar al-Assad amesema kuwa, endapo Wamagharibi wataiahidi na kuihakikishia Syria kwamba, wataacha kuwaunga mkono magaidi, basi serikali ya Damascus iko tayari kushirikiano nao

No comments:

Post a Comment