Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Sunday, 26 April 2015

Waburkinabe waunga mkono sheria mpya za uchaguzi

Maelfu ya wakazi wa mji mkuu wa Burkina Faso, Ouagadougou, waliandamana jana kuunga mkono sheria mpya za uchaguzi.
Waandamanaji hao walipiga nara zinazounga mkono sheria mpya za uchaguzi zilizopasishwa na Bunge tarehe 7 mwezi huu wa Aprili. Sheria hizo mpya zinawazuia wanachama wa serikali iliyoondoka madarakani kushiriki katika uchaguzi ujao.
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Burkina Faso, Auguste Denise Barry amesema kuwa serikali ya mpito ya nchi hiyo ina azma ya kukamilisha kipindi cha mpito kwa mafanikio.
Kwa mujibu wa sheria mpya za uchaguzi za Burkina Faso, mbali na kambi ya rais wa zamani wa nchi hiyo Blaise Compaoré, vyama vyote ambavyo viliunga mkono mpango wa kiongozi huyo wa kubadili katiba ili kumruhusu agombee tena kiti cha rais kwa zaidi ya mara mbili, vitazuiwa kushiriki katika uchaguzi ujao. Blaise Compaoré alilazimika kung'atuka madarakani Oktoba mwaka jana baada ya kushadidi wimbi la maandamano ya wananchi waliokuwa wakipinga utawala wake

No comments:

Post a Comment