Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Saturday, 25 April 2015

Boko Haram waushikilia tena mji wa Marte, Nigeria

Wanamgambo wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram wamewalazimisha mamia ya askari wa Nigeria kuukimbia mji wa mpakani wa Marte ulioko kwenye fukwe za Ziwa Chad. Kwa mujibu wa Imamu Habeeb, ambaye ni kiongozi wa eneo hilo pamoja na mashuhuda wa tukio hilo magaidi wa Boko wapatao 2,000 walichomoza kutokea pande tofauti na kupambana na askari wa jeshi la Nigeria.  Kwa mujibu wa bwana Habeeb mapigano hayo yalizuka siku ya Alkhamisi usiku na kuendelea hadi jana. Shehu Dan Baiwa, ambaye ni mmoja wa wanamgambo wa kujitolea katika jimbo la Borno amesema idadi ya wapiganaji hao wa Boko Haram ilikuwa zaidi ya elfu mbili wakiwa wamejizatiti kwa mabomu na vifaru. Amesema wanamgambo hao walikuwa wakifyatua risasi ovyo na kuua watu kadhaa. Hii ni mara ya tatu kwa kundi la kigaidi la Boko Haram kuushikilia tena mji wa Marte katika jimbo la Borno ambalo ni kitovu cha uasi wa kundi hilo unaoendelea kwa mwaka wa sita sasa na kusababisha vifo vya watu 13,000 na wengine milioni moja na nusu kubaki bila makaazi. Marte ulikuwa mmoja wa miji kadhaa iliyokombolewa na jeshi la Nigeria katika wiki za hivi karibuni lililoanzisha operesheni maalumu dhidi ya Boko Haram kwa msaada wa majeshi ya Chad, Cameroon na Niger. Mwanasiasa mmoja wa mji wa Marte ambaye hakutaka jina lake litajwe amethibitisha kushikiliwa tena mji huo na magaidi wa kundi la kitakfiri la Boko Haram. “Tumepoteza watu wengi, kwa sababu baadhi ya watu wetu waliokuwa wamekimbilia Chad walirudi baada ya askari wa Nigeria kuukomboa mji hivi karibuni” ameeleza mwanasiasa huyo. Hata hivyo afisa mmoja wa jeshi la Nigeria aliyethibitisha kutokea shambulio hilo la Boko Haram katika mji wa Marte amekataa kusema kuwa mji huo umeshikiliwa tena na kundi hilo na kueleza kwamba kuondoka kwa jeshi kumefanyika katika sura ya mbinu na mkakati wa kivita…/

No comments:

Post a Comment