Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Sunday, 26 April 2015

UNAMID yakadhibisha madai ya serikali ya Sudan

Kikosi cha askari wa kulinda amani cha Umoja wa Mataifa katika eneo la Darfur huko magharibi mwa Sudan (UNAMID) kimekanusha madai yaliyotolewa na serikali ya Khartoum dhidi ya askari wa kikosi hicho.
UNAMID imekanusha madai kwamba askari wake waliua raia katika mji wa Kaas huko kusini mwa Darfur na kusisitiza kuwa kikosi hicho kilijibu mashambulizi katika hali ya kujihami.
Afisa mwandamizi wa UNAMID amesema si sahihi kuwatuhumu askari wa kikosi cha kimataifa kwamba wameua raia na kwamba lengo la kutolewa tuhuma kama hizo ni kupotosha fikra za waliowengi nchini Sudan.
Jana Jumamosi Gavana wa jimbo la Darfur ya Kusini nchini Sudan aliwatuhumu askari wa vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa katika eneo la Darfur UNAMID kuwa wameua raia saba wasio na hatia katika jimbo hilo. Gavana Adam Jarunnabiy alisema kumeundwa tume maalumu ya kuchunguza mauaji ya raia hao

No comments:

Post a Comment