Jumuiya ya Madaktari Wasio na Mipaka imetahadharisha
juu ya kuzidi kuwa mbaya hali ya mambo ya mji wa Aden huko kusini mwa
Yemen, huku Saudi Arabia ikishadidisha mashambulilzi yake ya anga dhidi
ya nchi hiyo ya Kiarabu. Jumuiya ya Madaktari Wasio na Mipaka(MSF)
imetoa tahadhari hiyo Jumanne hii ikisema kuwa hali ya mambo katika mji
wa Aden inazidi kuwa mbaya siku baada ya siku. Mji wa Aden umegeuka na
medani ya mapigano makali kati ya vikosi vitiifu kwa Rais wa Yemen
aliyejiuzuluAbdurabbuh Mansour Hadi na wanachama wa makundi ya wananchi
wanaoungwa mkono na wapiganaji wa Kihouthi. Watu wanaoshuhudia mapigano
hayo wamesema kuwa vikosi vya majini vya Saudia vimeyashambulia maeneo
ya wanamapinduzi katika mji wa Aden, suala lililokanushwa na Saudi
Arabia.
No comments:
Post a Comment