Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Saturday, 25 April 2015

UNAMID watuhumiwa kuua raia saba Darfur, Sudan

Gavana wa jimbo la Darfur ya Kusini nchini Sudan amewatuhumu askari wa vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa katika eneo la Darfur UNAMID kuwa wameua raia saba wasio na hatia katika jimbo hilo. Adam Jarunnabiy, amesema askari wa UNAMID wamewaua kwa kuwapiga risasi raia saba wasio na ulinzi katika eneo la Kaas jimboni humo. Ameongeza kuwa tayari tume ya kuchunguza mauaji ya raia hao saba wa Sudan imeshaundwa. Kwa mujibu wa  gavana huyo wa Darfur ya Kusini, kundi la waasi lilipora gari moja la vikosi vya kulinda amani vya UNAMID na kwamba wakati askari wa vikosi hivyo waliopokuwa wakiwafukuza waasi hao waliwafyatulia risasi na kuwaua raia ambao walikuwa hawahusiki kwa namna yoyote ile na tukio la wizi wa gari hilo. Kumekuwepo na malalamiko mengi ya raia wa Sudan kuhusiana na uwezo wa vikosi vya UNAMID katika kulinda amani na kudhamini usalama wa raia hao kiasi cha kuifanya serikali ya Khartoum iutake Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa ziviondoe vikosi hivyo nchini humo. Darfur ya Kusini ni moja ya majimbo matano yanayounda eneo la Darfur lililoko magharibi mwa Sudan. Darfur ni eneo lenye utajiri mkubwa wa mafuta na maliasili nyenginezo yakiwemo madini ya urani na dhahabu, suala ambalo limesababisha kuzuka uasi wa utumiaji silaha ulioanza tangu mwaka 2003 na kuendelea hadi sasa…

No comments:

Post a Comment