Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 20 April 2015

Watu 11 wahukumiwa kifo machafuko ya soka Misri

Mahakama moja nchini Misri imewahukumu adhabu ya kifo watu 11 baada ya kuwapata na hatia ya kushiriki katika machafuko ya kwenye uwanja wa mpira katika mji wa Port Said, miaka mitatu iliyopita. Hukumu hiyo imetolewa leo kuhusiana na machafuko hayo ya mwaka 2012 ambayo yalipelekea watu 74 kuuawa. Hukumu iliyotolewa mwezi Februari 2014 na mahakama moja ya chini dhidi ya watuhumiwa 73 ilikatiwa rufaa baada ya kuwahukumu kifo watu 21 kwa kosa la kushiriki kwenye machafuko hayo. Hukumu ya adhabu ya kifo dhidi ya mashabiki 11 wa mpira imepelekwa kwa Mufti Mkuu wa Misri na mahakama itaamua hatima yao pamoja na hatima ya watuhumiwa wengine, Mei 30 mwaka huu. Mashabiki wenye misimamo mikali mara nyingi huwa wanapambana na polisi wakati wa mechi nchini Misri. Machafuko ya mwezi Februari 2012 yalitokea wakati mashabiki wa timu mwenyeji ya al Masry walipopambana na mashabiki wa timu ya al Ahly ya Cairo wakati wa mechi ya timu hizo mbili. Hata mwanzoni mwa mwezi Februari mwaka huu pia, watu kadhaa waliuawa baada ya kutokea machafuko kati ya mashabiki na polisi wakati wa mechi kati ya timu ya Zamalek na ile ya Enppi, mjini Cairo

No comments:

Post a Comment