Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Tuesday, 21 April 2015

S/Kusini yajiandaa na vita vya muda mrefu na waasi


Jeshi la Sudan Kusini limetangaza kuwa, linajiandaa na vita vya miaka kumi dhidi ya waasi katika nchi hiyo changa zaidi barani Afrika. Makamanda wa jeshi la Sudan Kusini wakishirikiana na wenzao wa jeshi la UgandaUPDF wamo katika maandalizi ya vita vya miaka kumi dhidi ya makundi ya waasi. Makamanda wa jeshi la Sudan Kusini wanatabiri kwamba, waasi wanaoongozwa na Riek Machar aliyekuwa makamu wa Rais wa Sudan Kusini hawatasalimu amri kwa haraka hivyo jeshi la nchi hiyo linapaswa kuweka malengo ya vita ya miaka kumi. Jeshi la Sudan Kusini limekuwa likisaidiwa na jeshi la Uganda UPDF katika juhudi za kuwatokomeza waasi wa nchi hiyo wanaoongozwa na Riek Machar. Hayo yanajiri katika hali ambayo, Umoja wa Afrika unaendelea na upatanishi wake wa mgogoro wa Sudan Kusini ambapo siku ya Jumamosi uliitisha mkutano wa pande mbili hasimu za nchi hiyo. Umoja wa Afrika ulipendekeza katika mkutano huo kwamba, pande mbili hasimu huko Sudan Kusini kila mmoja upatiwe asilimia 40 ya madaraka, asilimia kumi ipewe miungano na vyama vya kisiasa na asilimia kumi iliyobakia apewe Pagan Amum, Katibu Mkuu wa zamani wa chama tawala.

No comments:

Post a Comment