Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Tuesday, 21 April 2015

Wapinzani wamteua Mutabazi kuwania urais Burundi


Mrengo wa upinzani nchini Burundi unaoundwa na vyama tisa, umemtangaza Jean de Dieu Mutabazi kuwa ndiye atayapeperusha bendera yao katika uchaguzi ujao wa rais nchini humo. Muungano huo unaojulikana kwa jina la Participatory Opposition Coalition in Burundi COPA kwa kifupi umetangaza kuwa, umemteua Jean Mutabazi kuwa mgombea wake katika uchaguzi ujao wa Rais nchini Burundi uliopangwa kufanyika Juni mwaka huu. Jean Mutabazi ambaye pia ndiye mwenyekiti wa muungano huo wa COPA amesema kuwa, muungano huo wa vyama vya upinzani haumuhofii mgombea yeyote yule akiwemo wa chama tawala CNDD-FDD Rais Pierre Nkurunziza. Muungano wa COPA uliundwa Septemba mwaka jana na umejindaa kushiriki vizuri katika uchaguzi mkuu ujao nchini Burundi. Wiki iliyopita pia chama cha The National Rally for Change RANAC kwa kifupi kilimtangaza Rais wa zamani wa nchi hiyo Domitien Ndayizeye kuwa mgombea wake katika uchaguzi ujao wa Rais nchini Burundi. Aidha chama cha FRODEBU kwa upande wake nacho kimemteua Dr Jean Minani kuwa mgombea wake wa kiti cha urais katika uchaguzi ujao

No comments:

Post a Comment