Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Wednesday, 8 April 2015

Afrika K, yamnasa binti aliyetaka kujiunga na Daesh

Maafisa wa Afrika Kusini wamemtia mbaroni binti mwenye umri wa miaka 15 aliyekuwa amepanga kuondoka nchini humo kwa lengo la kujiunga na kundi la wanamgambo wa kitakfiri la Daesh huko Syria.  Binti huyo ambaye jina lake halikufahamika alinaswa Jumapili wiki hii katika uwanja wa ndege wa mjini Cape Town. Binti huyo alikutwa katika ndege ya shrike la ndege la Uingereza akiwa ameketi ndani ya katika sehemu inayojulikana  kama "business class" kwa ajili ya kuelekea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Oriver Tambo huko Johannesburg.  Binti huyo mweney umri wa miaka 15 alipanga kuelekea Uturuki kwa kutumia usafiri wa ndege, na kisha kusafiri kwa kutumia baraka ili kuelekea Syria kwa minajili ya kujiunga na Daesh. Ndugu na wazazi wa mtoto huo wamesema kuwa mwezi uliopita binti wao ajiingiza sana katika masuala ya kisiasa.

No comments:

Post a Comment