Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullahil Udhma
Sayyid Ali Khamenei ametoa msamaha na punguzo la adhabu kwa iddai kadhaa
ya wafungwa wanawake kwa mnasaba wa maadhimisho ya kuzaliwa Bibi Fatma
Zahra (as) binti Mtukufu wa Mtume Muhammad (saw). Kiongozi Muadhamu
ametoa msamaha na punguzo hilo la adhabu baada ya kuafiki ombi la
Ayatullah Sadiq Amoili Larijani Mkuu wa Vyombo vya Mahakama hapa nchini
aliyewasilishwa kwake akitaka kusamehewa na kupunguziwa adhabu idadi
kadhaa ya wafungwa wanawake waliotimiza masharti ya kupatiwa msamaha au
punguzo hilo. Ikumbukwe kuwa, Waislamu hususan wa madhehebu ya Shia
katika maeneo mbalimbali duniani tangu jana usiku walianza kuadhimisha
tukio la kuzaliwa binti wa Mtume wetu Muhammad (saw), Bibi Fatimatu
Zahra (as) linalosadifiana na siku ya leo ya tarehe 20 Mfunguo Tisa
Jamadithani. Sherehe hizo zinafika kileleni leo kwa kufanyika vikao vya
mihadhara na majlisi za sherehe zinazotumbuizwa kwa tungo za kumsifu
Mtume (saw), binti yake mtukufu na Ahlibaiti zake watoharifu. Siku ya
kukumbuka kuzaliwa mwanamke bora kuliko wote duniani, yaani Fatima binti
Muhammad (saw) hapa nchini Iran inasherehekewa kama Siku ya Mama,
ambapo akina mama huenziwa na kutunzwa.
No comments:
Post a Comment