Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Thursday, 23 April 2015

saudia ingali inaendeleza mashambulizi dhidi ya Yemen

Ndege za kivita za Saudi Arabia zimeendeleza mashambulizi yake ya kichokozi katika maeneo tofauti ya Yemen ikiwemo miji ya Hajja na Taiz na maeneo mengine ya nchi hiyo. Aidha ndege za kivita za utawala wa Aal Saudi zimetekeleza mashambulizi makali dhidi ya mji wa al-Dhahir uliopo katika mkoa wa Saada na kupelekea watu wengi kuuawa na kujeruhiwa. Hii ni katika hali ambayo, wanamapambano wa Yemen kwa kushirikiana na jeshi la nchi hiyo wamefanikiwa kudhibiti kambi ya jeshi ya kikosi cha 35 iliyokuwa ikidhibitiwa na magaidi wa al Qaeda katika mkoa wa Taiz ambapo wamefanikiwa pia kuwafurusha matakfiri hao kutoka eneo hilo. Aidha wanamapambano wa Yemen wamedhibiti ngome muhimu za magaidi wa kitakfiri katika mji wa Marib na eneo la al-Wahat katika mkoa wa Hajja. Kwa mujibu wa duru za habari, ndege za Saudia na waitifaki wake zimeshambulia ngome hizo za magaidi muda mchache tu baada ya kudhibitiwa na wanamapambano kwa kushirikiana na jeshi la Yemen. Mashuhuda wamenukuliwa wakisema kuwa, magaidi hao wanaoungwa mkono na Saudia, wamebaki wakikimbia mitaani huku na kule kufuatia kupokonywa ngome zao walizokuwa wakizitumia katika kutekeleza mashambulizi na njama dhidi ya taifa hilo la Kiarabu. Mashambulizi hayo ya ndege za utawala wa Aal Saudi yanajiri katika hali ambayo siku mbili zilizopita muungano wa nchi zinazoshirikiana na Riyadh katika hujuma nchini Yemen, zilikuwa zimetangaza kuhatimisha operesheni hizo

No comments:

Post a Comment