Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Tuesday, 21 April 2015

Makundi hasimu yasimamisha vita mjini Sirte, Libya

Makundi hasimu nchini Libya yameanza kutekeleza makubaliano ya kusimamisha vita kwa muda wa siku kumi katika mji wa bandari wa Sirte wa kaskazini mwa nchi hiyo. Gazeti la Bawwabatul Wasat la Libya limeripoti kuwa, lengo la usimamishaji vita huo wa muda ulioanza jana Jumatatu ni kutoa fursa ya kufanya mazungumzo na kundi la kitakfiri la Daesh. Kwa mujibu wa gazeti hilo, makundi yote yanayohusika na mgogoro wa Libya yamekubaliana na usitishaji vita huo. Huku hayo yakiripotiwa, taarifa nyingine zinasema kuwa, kumetokea mripuko wa bomu kwenye ubalozi wa Uhispania huko Tripoli, mji mkuu wa Libya. Hata hivyo hakuna taarifa zozote zilizotolewa kuhusiana na hasara kamili zilizosababishwa na mripuko huo uliotokea usiku wa kuamkia leo. Taarifa za awali zinasema kuwa mripuko huo umesababisha uharibifu katika eneo la ubalozi huo na kwenye majengo jirani. Kundi la kigaidi la Daesh ndilo linalonyooshewa kidole cha lawama kutokana na kufanya mashambulizi kama hayo ya kuwalenga wageni nchini Libya kwa muda mrefu sasa.

No comments:

Post a Comment