Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 13 April 2015

Kamishna wa Haki za Binadamu wa UN yuko Burundi

Zeid Ra'ad al Hussein Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amewasili nchini Burundi kwa lengo la kukutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa ngazi za juu wa nchi hiyo. Zeid Ra'ad al Hussein anayefanya safari hiyo ya siku tatu nchini Burundi, atakutana na kufanya mazungumzo na Rais Pierre Nkurunziza na viongozi wengine wa ngazi za juu wa nchi hiyo. Miongoni mwa ratiba alizopangiwa nchini humo, ni pamoja na kushiriki kwenye mdahalo unaohusiana na masuala ya haki za binadamu nchini Burundi na zoezi la uchaguzi wa rais uliopangwa kufanyika mwezi Juni mwaka huu. Umoja wa Mataifa umeeleza kuwa, hali ya kisiasa na haki za binadamu nchini Burundi ni ya kusikitisha. Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ambaye ni raia wa Jordan alichukua wadhifa huo mwaka jana, na hii ni mara ya kwanza kwa mkuu wa taasisi hiyo ya kimataifa kushikiliwa na Mwislamu.

No comments:

Post a Comment