Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 27 April 2015

HRW: Kesi ya dhidi ya Mursi ilikuwa na dosari

Shirika la Kutetea Haki za Binadamu(HRW)  limekosoa mamlaka husika za Misri kwa kuendesha kesi isiyo ya kiadilifu na chuki kwa Rais wa nchi hiyo aliyepinduliwa na jeshi, likisema kuwa upande wa uendeshaji wa mashtaka uligubikwa na dosari. Taarifa iliyotolewa Jumapili hii na Human Rights Watch imeeleza kuwa kesi ya Mohamed Morsi iligubikwa na mchakato wa ukengeukaji wa kanuni, chuki na ukosefu wa ushahidi wenye kuthibitisha. Taarifa ya Shirika la Kutetea Haki za Binadamu imeongeza kuwa, upande wa mashtaka ulitegemea sana ushahidi uliotolewa na maafisa wa kijeshi na polisi na kwamba kesi hiyo dhidi ya Mursi ilichochewa kisiasa dhidi ya harakati ya Ikhwanul Muslimin ya Misri. Sarah Leah Whitson Mkurugenzi Mkuu wa Human Rights Watch katika eneo la Mashariki ya Kati na Kaskazini mwa Afrika amesema kuwa Mursi alitajwa kuhusika katika kesi kwa sababu tu ya uhusiano kati yake na harakati ya Ikhwanul Muslimin. Bi Whitson amewatuhumu waendesha mashtaka waliomhukumu Mursi katika kesi ya hivi karibuni kuwa walipuuza vifo vya wafuasi wa Ikhwanul Muslimin katika ghasia za mwaka 2012 na kutojali kushindwa vikosi vya usalama kuchukua hatua wakati wa ghasia hizo

No comments:

Post a Comment