Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 10 April 2015

Morocco yaijia juu AU kuhusu Sahara Magharibi

Serikali ya Morocco imesisitiza upinzani dhidi ya hatua yoyote ile ya Umoja wa Afrika ya kutaka kusaidia kuipatia ufumbuzi kadhia ya Sahara Magharibi. Hayo yameelezwa na SalaheddineMezouar, Waziri wa Mashauri ya Kigeni na Ushirikiano wa Morocco ambaye amesisitiza kwamba, nchi yake inapinga kadhia ya Sahara Magharibi kuingiliwa na Umoja wa Afrika. Salaheddine Mezouar amesema hayo ikiwa ni radiamali kwa matamshi ya Mkuu wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika aliyesema katika barua yake kwa Ban Ki-Moon Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa kwamba, kuna udharura wa kuweko himaya ya haki za binadamu ya vikosi vya kusimamia amani katika eneo la Sahara Magharibi. Waziri wa Mashauri ya Kigeni na Ushirikiano wa Morocco amesema kwamba, barua ya hivi karibuni ya Baraza la Usalama la Amani la Umoja wa Afrika kuhusiana na kadhia ya Sahara Magharibi ilionyesha jinsi Umoja wa Afrika unavyoegemea upande mmoja katika kadhia hiyo. Ni kutokana na sababu hiyo ndiyo maana serikali ya Rabat inapinga vikali Umoja wa Afrika kuwa na nafasi yoyote ile katika kadhia ya Sahara Magharibi, amesisitiza waziri huyo wa mashauri ya kigeni wa Morocco.

No comments:

Post a Comment