Umoja wa Mataifa umeeleza wasiwasi wake juu ya kusahaulika
mgogoro wa Jamhuri ya Afrika ya Kati. Ripoti iliyotolewa na Shirika la
Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) imesema kuwa, idadi ya
wakimbizi laki tisa wa nchi hiyo ambalo ni tatizo mkubwa la kibinaadamu,
ni suala ambalo halitakiwi kusahaulika wala kupuuzwa na jamii ya
kimataifa. Ripoti hiyo imeeleza kuwa, zaidi ya raia laki nne na 60 elfu
wa Jamhuri ya Afrika ya Kati wamekimbilia nje ya nchi, huku wengine
wapatao laki nne na elfu 36 wakiwa wakimbizi wa ndani. UNHCR imesisitiza
kuwa, karibu watu milioni mbili na laki saba wanahitajia msaada wa
haraka kutokana na hali yao mbaya. Imeongeza kuwa, licha ya kiwango
hicho cha kutia wasiwasi lakini bado asasi husika zimeshindwa kudhamini
bajeti kwa ajili ya misaada ya waathirika hao wa mgogoro wa Jamhuri ya
Afrika ya kati.
Mgogoro wa Jamhuri ya Afrika ya Kati ulishadidi zaidi mnamo mwaka 2013, baada ya kuondolewa madarakani aliyekawa rais wa nchi hiyo, Francois Bozize na waasi wa muungano wa Seleka. Mgogoro ulifuatiwa na mauaji makubwa, ambayo wahanga wake wengi walikuwa Waislamu.
Mgogoro wa Jamhuri ya Afrika ya Kati ulishadidi zaidi mnamo mwaka 2013, baada ya kuondolewa madarakani aliyekawa rais wa nchi hiyo, Francois Bozize na waasi wa muungano wa Seleka. Mgogoro ulifuatiwa na mauaji makubwa, ambayo wahanga wake wengi walikuwa Waislamu.
No comments:
Post a Comment