Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Sunday, 26 April 2015

Magaidi wazidi kutwangana wenyewe nchini Syria

Habari kutoka nchini Syria zinasema kuwa mapigano baina ya makundi ya kigaidi yamepamba moto nchini humo. Mtandao wa habari wa an Nashrah wa nchini Lebanon umetangaza kuwa, leo Jumapili, wanamgambo wa kundi la kigaidi la Daesh wametwangana na makundi mengine kadhaa ya kigaidi katika mji wa Mari' mkoani Halab, kaskazini mwa Syria. Kwa mujibu wa mtandao huo makumi ya magaidi wameuawa kwenye mapigano hayo. Wakati huo huo jeshi la Syria leo limeendeleza operesheni zake za kukomboa maeneo mbalimbali kutokana mikononi mwa makundi ya kigaidi yakiwemo maeneo ya Jisrush Shughur huko Idlib, kaskazini magharibi mwa Syria na kufanikiwa kuyasafisha kikamilifu maeneo hayo kutoka mikononi mwa magaidi wanaoungwa mkono na madola ya kigeni na ya kibeberu kama vile utawala wa Kizayuni wa Israel. Habari nyingine kutoka Syria zinasema kuwa, leo Jumapili, kundi la kigaidi la Jabhatun Nusra limewaua kwa umati wananchi 30 wa Syria katika eneo la Jisrush Shughur huko Idlib, ikiwa ni kuendeleza jinai zake za kila leo dhidi ya wananchi wa Syria

No comments:

Post a Comment