Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Tuesday, 28 April 2015

hadi kufikia sasa waliouawa kwa mtetemeko wa ardhi Nepal wafikia 3800

Idadi ya watu waliopoteza maisha katika tetemeko la ardhi nchini Nepal imeongeza na kufikia 3800, kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi hiyo. Wizara hiyo imetangaza kuwa, zaidi ya watu 7000 wamejeruhiwa na wengi wao wako katika hali mahututi. Rameshwor Dangal, mkuu wa Idara ya Kupambana na Majanga iliyo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nepal, amethibitisha habari hiyo na kuongeza kuwa, watu wengine 90 kati ya wahanga hao, walipoteza maisha nchi jirani hususan, China na India ambazo nazo zilikumbwa na mtetemeko huo. Tetemeko la ardhi lililotokea juzi nchini Nepal lilikuwa na ukubwa wa 7,8 kwa kipimo cha rishta, na halijawahi kushuhudiwa nchini humo kwa kipindi cha miongo minane iliyopita. Tetemeko hilo lilisababisha pia kuporomoka theluji ya mlima Everest na kuua watu wanamichezo 18 wa skii.
Tayari Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametuma salamu za rambirambi kwa Rais wa Nepal, Ram Baran Yadav kutokana na maafa hayo

No comments:

Post a Comment