Wakazi wa mji wa Baltimore nchini Marekani wamefanya maandamano
wakitaka kutendewa haki na uadilifu Mmarekani mweusi aliyefariki dunia
baada ya kujeruhiwa akiwa mikononi mwa polisi.
Waandamanaji hao walibeba mabango yenye maandishi: "Maisha ya Watu Weusi Yana Thamani". Vilevile wametaka kukomeshwa ubaguzi dhidi ya Wamarekani wenye asili ya Afrika unaofanywa na vyombo vya dola. Waandamanaji hao pia wametaka kutendewa haki Mmarekani mweusi, Freddie Gray, ambaye amefariki dunia Jumapili iliyopita akiwa hospitalini baada ya kujeruhiwa na polisi ya Marekani. Uchunguzi wa maiti ya mhanga huyo umebaini kuwa Freddie Gray alifariki dunia kutokana na majeraha makali kwenye uti wa mgongo. Mwanasheria wa familia ya Gray anasema kijana huyo aliyekuwa na umri wa miaka 25 alipoteza fahamu na baadaye kufariki dunia baada ya kuvunjwa uti wa mgongo akiwa katika korokoro ya Polisi ya Marekani
Waandamanaji hao walibeba mabango yenye maandishi: "Maisha ya Watu Weusi Yana Thamani". Vilevile wametaka kukomeshwa ubaguzi dhidi ya Wamarekani wenye asili ya Afrika unaofanywa na vyombo vya dola. Waandamanaji hao pia wametaka kutendewa haki Mmarekani mweusi, Freddie Gray, ambaye amefariki dunia Jumapili iliyopita akiwa hospitalini baada ya kujeruhiwa na polisi ya Marekani. Uchunguzi wa maiti ya mhanga huyo umebaini kuwa Freddie Gray alifariki dunia kutokana na majeraha makali kwenye uti wa mgongo. Mwanasheria wa familia ya Gray anasema kijana huyo aliyekuwa na umri wa miaka 25 alipoteza fahamu na baadaye kufariki dunia baada ya kuvunjwa uti wa mgongo akiwa katika korokoro ya Polisi ya Marekani
No comments:
Post a Comment