Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 27 April 2015

Zarif: Hitilafu za ndani Marekani hazizuii makubaliano

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kuwa, kwa mtazamo wa Iran, serikali ya Marekani ndiye inayopasa kutekeleza makubaliano ya nyuklia na kwamba hitilafu za ndani za nchi hiyo haziizuii nchi hiyo kutotekeleza ahadi na makubaliano yake ya kimataifa. Muhammad Javad Zarif amesema kuhusiana na baadhi ya makelele yaliyozushwa ndani ya Congresi ya Marekani na mivutano kati ya vyama viwili vya nchi hiyo kuhusu makubaliano ya nyuklia na Iran na kueleza kuwa: Iran inaitambua serikali ya Marekani kuwa ndiyo inayopasa kutekeleza makubaliano na kwamba matatizo na mivutano ya ndani ya Marekani haiihusu Iran wala suala la utekelezaji wa makubaliano hayo. Amesema kwa mujibu wa sheria za kimataifa, matatizo ya ndani ya nchi, hayatoi kisingizio kwa  nchi hizo kutotekeleza makubaliano yake ya kimataifa.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameyasema hayo jana alasiri kwa wakati wa New York Marekani.
Muhammad Javad Zarif amelitaja lengo kuu la safari yake huko New York kuwa ni kwa ajili ya kushiriki katika mkutano wa kuangalia upya mkataba wa NPT

No comments:

Post a Comment