Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Sunday, 26 April 2015

Onyo la Naibu Waziri Mambo/Nje wa Iran kwa Saudia

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayeshughulikia masuala ya Kiarabu na Kiafrika ameilaumu Saudi Arabia kwa kuzuia misaada ya kibinadamu ya Iran isiwafikie wananchi wa Yemen. Hussein Amir Abdollahiyan amesema hayo leo na kuongeza kuwa, vitendo vya Saudia vya kuizingira Yemen na kuzuia misaada ya kibinadamu ya Iran kuwafikia wananchi wa nchi hiyo havitaachwa vipite vivi hivi. Ameongeza kuwa, daima Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekuwa ikihimiza kutumiwa njia za mazungumzo na kidiplomasia kutatua masuala mbalimbali hata hivyo ametahadharisha kuwa, Iran inazingatia machaguo yote kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wa Yemen, kuwatumia misaada ya haraka ya kibinadamu na kuchukua majeruhi wa nchi hiyo kwa ajili ya kuwatibu. Vile vile amesema kuwa, Saudia haina haki ya kuwapangia cha kufanya watu wengine na kuonya kuwa, uingiliaji wa kijeshi wa Saudia nchini Yemen ambao umeshapelekea mamia ya watu kuuawa na maelfu ya wengine kujeruhiwa sambamba na kuharibiwa miundombinu ya nchi hiyo ya Kiarabu, utapelekea kuwa mkubwa zaidi mgogoro wa Yemen kwa madhara ya eneo hili zima kwani hadi hivi sasa matokeo ya uvamizi huo si kitu kingine ghairi ya ukosefu wa amani ndani ya Saudia kwenyewe na katika eneo hili lote kiujumla

No comments:

Post a Comment