Umoja wa Mataifa umetoa ripoti kuhusu kuongeza jinai za utawala wa
Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina. Ripoti ya kila wiki ya Taasisi
ya Kimataifa ya Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa
Mataifa huko Palestina imeonyesha kuwa, wanajeshi wa utawala wa Kizayuni
wiki iliyopita walizishambulia mara 110 nyumba za raia wa Kipalestina
katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kuwateka nyara Wapalestina
132. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, katika muda wa wiki hiyo moja
Wapalestina 64 wakiwemo watoto 5 walijeruhiwa katika maeneo mbalimbali
ya ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na kijana wa Kipalestina
aliyejeruhiwa wiki iliyopita na wanajeshi wa Kizayuni ameaga dunia.
Katika kipindi hicho cha wiki moja iliyopita, nyumba tatu mali za
Wapalestina zilibomolewa pia na wanajeshi wa Israel katika kijiji
kimoja karibu na mji wa Jenin.
Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa vile vile imetangaza kuwa kivuko cha Rafah ambacho ni njia pekee inayotegemewa na raia wa Palestina wa Ukanda wa Ghaza ili kuwasiliana na ulimwengu wa nje, kilitaka pia kufungwa wakati fulani
Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa vile vile imetangaza kuwa kivuko cha Rafah ambacho ni njia pekee inayotegemewa na raia wa Palestina wa Ukanda wa Ghaza ili kuwasiliana na ulimwengu wa nje, kilitaka pia kufungwa wakati fulani
No comments:
Post a Comment