Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 10 April 2015

Kongamano la kimataifa la Qur'ani laendelea Morocco

Kongamano la tatu la kimataifa la watafiti na wasomi wakubwa wa Qur'ani Tukufu limeendelea leo kwa siku yake ya pili huko mjini Fez, Morocco. Kongamano hilo lililoanza jana na ambalo linajadili kadhia ya uandishi wa elimu ya misingi ya tafsiri, matukio na malengo, linahudhuriwa na idadi kubwa ya maulamaa, watafiti wakubwa wa elimu ya Qur'ani na wataalamu wa nadharia wa Vyuo Vikuu vya Kiislamu katika fani ya Tafsiri ya Qur'ani, kutoka Morocco na nchi nyengine za Kiislamu. Aidha kongamano hilo la siku tatu, mbali na kujadili kadhia ya uandishi wa misingi ya tafsiri, litajadili pia masuala kwa ujumla ya uandishi wa elimu ya tafsiri, ikiwemo msingi wa kutegemea vyanzo vikuu ambavyo, ni Qur'ani na hadithi sahihi za Mtume, maana na lugha ya tafsiri ya Qur'ani, mambo ambayo yanapewa kipaumbele zaidi na watafiti wa kielimu kwa ajili ya kutoa mwanya wa kufanyika uchunguzi zaidi wa kitabu hicho cha Allah. Kando na kongamano hilo, kunafanyika pia maonyesho mbalimbali ya Qur'ani kwa kuwajumuisha magwiji na weledi wa masuala ya kidini na pia maonyesho ya vitabu mbalimbali vya

No comments:

Post a Comment