Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Sunday, 26 April 2015

Kiongozi Muadhamu: Iran haitaki polisi ya ki-Hollywood

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, jeshi la polisi ni dhihirisho la nguvu za utawala na usalama za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Ayatullahil Udhma Sayyid Ali Khamenei amesema hayo leo Jumapili wakati alipoonana na washiriki wa kongamano la makamanda, wakuu na wakurugenzi wa Jeshi la Polisi la Iran na kusisitiza kuwa, miongoni mwa majukumu makuu ya polisi ni kudhamini usalama wa watu binafsi, wa kijamii, wa kimaadili, wa kiroho na wa kisaikolojia katika jamii.
Ameongeza kuwa, jeshi la polisi linapaswa kuwa chombo chenye nguvu ili liweze kulinda usalama lakini nguvu hizo zinapaswa kuchunga uadilifu, murua na huruma.
Aidha amesema, vituko vinavyofanywa barabarani na baadhi ya vijana waliolewa ghururi za utajiri kwa kutumia magari ya kifakhari ni aina moja ya kuhatarisha usalama wa kisaikolojia katika jamii na kusisitiza kuwa: Jeshi la Polisi linapaswa kupambana na vitendo vya aina zote vya kuhatarisha amani.
Ayatullahil Udhma Khamenei amesisitiza pia kuwa Iran haitaki kuwa na nguvu za jeshi la ki-Hollywood na za jamii za Magharibi na Marekani na kubainisha kwamba: Nguvu za aina hiyo si tu kwamba haziwezi kudhamini usalama, bali zenyewe ni aina moja ya mambo yanayohatarisha usalama.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amegusia pia namna polisi wa Marekani wanavyowakandamiza watu weusi nchini humo na kusema kuwa, huo ni moja ya mifano ya nguvu za kidhulma za polisi.
Ameongeza kuwa: Polisi wa Marekani wanawafanyia dhulma kubwa na kuwanyanyasa vibaya watu weusi licha ya kwamba rais wa hivi sasa wa nchi hiyo ni mtu mweusi, na vitendo hivyo bila ya shaka yoyote ndivyo vinavyopelekea kuzuka machafuko nchini humo

No comments:

Post a Comment