Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Tuesday, 21 April 2015

UN yalaani mauaji ya Daesh dhidi ya Waethiopia

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limelaani vikali mauaji ya kinyama yaliyofanywa na kundi la kigaidi la Daesh dhidi ya Wakristo 30 wa Ethiopia ambao waliuawa kinyama kwa kuchinjwa huko Libya. Taarifa ya wanachama 15 wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa imelaani vikali mauaji hayo na kubainisha kwamba, kitendo hicho cha Daesh kimethibitisha kwa mara nyingine tabia ya unyama na ukatili liliyo nayo kundi hilo. Baraza la Usalama limesisitiza kuwa, jinai za Daesh hazina mpaka na kwamba, kundi hilo limekuwa likitenda jinai na mauaji bila ya kujali thamani za kiutu na kibinadamu; na hivyo kuwa adui wa mataifa yote. Taarifa ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa imebainisha kuwa, kuna haja ya kuchukuliwa hatua kali za kukabiliana na kundi hilo ambalo limekuwa likifanya mauaji ya kutisha. Kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh hivi karibuni lilitoa mkanda wa video unaoonyesha wanachama wa kundi hilo wakiwachinja Wakristo wasiopungua 30 raia wa Ethiopia nchini Libya. Mkanda huo wa video wa dakika 29 unaonyesha magaidi wa Daesh wakiwauwa kwa kuwachinja Wakristo 16 wa Ethiopia katika pwani moja huko Libya na kuwaua wengine kwa kuwapiga risasi katika eneo la jangwani.

No comments:

Post a Comment