Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Thursday, 23 April 2015

“Umasikini sababu ya uharibifu wa mazingira Tanzania"


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal amesema kuwa, uharibifu wa mazingira katika nchi zinazoendelea ni kati ya sababu zinazofanya nchi hizo ziendelee kuwa maskini. Dakta Gharib Bilal amesema kuwa, upo uhusiano mkubwa kati ya mazingira na umaskini kwa maana kwamba, uharibifu wa mazingira unachangia kuongezeka kwa umaskini na kwamba kadri hali ya umaskini inavyoongezeka inasababisha uharibifu wa mazingira. Makamu wa Rais wa Tanzania ameongeza kuwa, kwa msingi huo umuhimu wa kulinda na kuhifadhi mazingira nchini unachochewa zaidi na ukweli kwamba mazingira ni mhimili wa sekta za uzalishaji kama vile kilimo, utalii, uvuvi na madini. Aidha amebainisha kuwa, changamoto iliyopo ni kuhakikisha mazingira na maliasili za Tanzania zinatumika katika njia endelevu kwa kuzingatia uwiano mzuri kati ya matumizi ya maliasili, hifadhi zake na uwezo wake kuendelea kutoa huduma. Makamu huyo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amebainisha kuwa, ili kusimamia masuala ya hifadhi ya mazingira kwa ufanisi ni lazima kudhibiti shughuli za binadamu zinazoathiri mazingira, masuala ya kijamii na kiuchumi kama vile ongezeko la watu, na shughuli za kiuchumi zinazoendana na matumizi yasiyo endelevu ya mazingira zinazoweka shinikizo kubwa katika mazingira na kusababisha uharibifu.

No comments:

Post a Comment