Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 10 April 2015

Mashambulio ya Saudia Arabia yakata mawasiliano

Mashambulio ya anga ya Saudi Arabia yanayoendelea kushuhudiwa nchini Yemen licha ya malalamiko ya jamii ya kimataifa yamelenga mitambo na vituo kadhaa vya mawasiliamo magharibi na kaskazini magharibi mwa nchi hiyo. Waziri wa Usafiri wa Yemen amesema kuwa,  ndege za kijeshi za Saudia zimeshambulia na kulenga mitambo ya kurushia matangazo ya televisheni katika mji mkuu Sana’a na katika miji ya Sa’ada na Amran. Taarifa zaidi zinasema kuwa, mashambulio hayo yaliyofanywa kwa makusudi yalikusudia kukata nyenzo za mawasiliano zinazotumiwa na wanamapinduzi wa Harakati ya al-Houthi. Baadhi ya duru zinaripoti kwamba, mawasiliano ya simu yamevurugika huku huduma ya Intaneti ikikatika katika miji hiyo mitatu kufuatia mashambulio hayo yaliyolenga vituo na mitambo ya mawasiliano. Wakati huo huo mashirika mbalimbali ya utoaji misaada yametahadharisha kwa mara nyingine tena kwamba, mgogoro wa Yemen unaelekea pabaya kutokana na kuwa mbaya hali ya kibinadamu katika nchi hiyo.   Familia nyingi katika baadhi ya miji hazipati huduma muhimu kama maji, chakula na dawa, huku watoto wakiwa ndio wahanga wakuu wa mashambulio ya sasa ya anga ya Saudia huko Yemen, imebainisha taarifa ya mashirika hayo.

No comments:

Post a Comment