Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Wednesday, 29 April 2015

Palestina yakaribisha ripoti ya UN iliyoishutumu Israel

Waziri wa Mambo ya Nje wa Palestina amekaribisha ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyoshutumu mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika shule ya umoja huo katika eneo la Ukanda wa Ghaza.
Waziri wa mambo ya Nje wa Palestina Riyadh al Maliki Jumanne hii amekaribisha ripoti hiyo ya Umoja wa Mataifa iliyolaani mashambulizi ya Israel dhidi ya shule inayosimamiwa na Umoja wa Mataifa huko Ukanda Ghaza wakati wa mashambulizi ya siku 50 yaliyoanzishwa na Israel katika msimu wa joto mwaka uliopita na kusema kuwa, kopi ya ripoti hiyo itawasilishwa kwa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kwa ajili ya uchunguzi.
Riyadh al Maliki ameongeza kuwa, ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyoshutumu mashambulizi ya mwaka jana ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika shule ya UN huko Ghaza, inahusiana na uchunguzi wa awali ambao tayari umeanza katika mahakama ya ICC na kwamba ripoti hiyo itasaidia sana kupata matokeo. Waziri wa Mambo ya Nje wa Palestina amesisitiza ulazima wa kufanywa uchunguzi rasmi kuhusu mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel huko Ghaza na mauaji yaliyofanywa na utawala huo mtenda jinai dhidi ya raia wa Palestina wasio na hatia wa eneo hilo.
Maelfu ya wapealestina waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika mashambulizi hayo ya Israel

No comments:

Post a Comment