Hassan Nassor Moyo
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.
HASSAN Nassoro Moyo, ni kati ya waasisi wawili wa Muungano kwa upande wa Zanzibar ambao mpaka sasa bado wako hai. Mwingine ni Alhaj Aboud Jumbe Mwinyi.
Moyo ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 80, ni Waziri wa kwanza wa Sheria aliyekula kiapo cha utii na uaminifu mbele ya Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano, Hayati Mwalimu Julius Nyerere Aprili 27 mwaka 1964, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Yeye ni miongoni mwa wajumbe 20 kutoka Bara na Zanzibar walioongozwa na Hayati Shekhe Thabit Kombo kuunda Katiba ya Chama Cha Mapinduzi kilichozaliwa Mwaka 1977 ambapo Katiba hiyo ilifanyiwa marekebisho kidogo na kuzaa Katiba ya Muungano inayotumika sasa na ambayo ipo katika hatua za mchakato wa marekebisho yake.
No comments:
Post a Comment