Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Tuesday, 28 April 2015

Wanaharakati wakamatwa, ghasia zaendelea Burundi

Polisi ya Burundi leo imemkamata kinara wa wanaharakati wa kutetea haki za bininadamu nchiniu humo, Pierre-Claver Mbonimpa, kufuatia machafuko na maandamano yanayoendelea nchini humo kupinga uamuzi wa Rais Pierre Nkurunziza wa kogombea kiti cha rais kwa mara ya tatu.
Vilevile vyombo vya usalama vya Burundi vimetoa waranti wa kutiwa nguvuni Vital Nshimirimana ambaye ndiye anayeongoza kampeni ya kumzuia Mkurunzinza asiwania tena urais kwa awamu ya tatu.
Wakili wa Mbonimpa, Armel Niyongere, amesema mteja wake hakuelezwa tuhuma zinazomkabili na kwamba anaamini amekamatwa kutokana na kuwataka wananchi washiriki kwenye maandamano ya leo. Walioshuhudia wamesema polisi walimpiga makofi na mateke mwanaharakati huyo.
Ghasia na machafuko yameendelea leo nchini Burundi huku wananchi wakiandamana kupinga uamuzi wa chama tawala cha CNDD-FDD wa kumuidhinisha Mkurunziza kuwania tena kiti cha rais. Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu nchini Burundi Alexis Manirakiza amesema watu 6 waliuawa katika machafuko ya jana mjini Bujumbura.

No comments:

Post a Comment