Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Benjamin Mkapa
amezitaka nchi za Kiafrika kukuza uongozi bora na kuachana na mikataba
mibovu isiyojali ustawi wa wananchi kwa kuwa inaweza kuzipeleka katika
vita. Miongoni mwa mikataba ambayo Mkapa amesema kuwa ni mibovu na
isiyofaa, hivyo iepukwe ni wa Kiuchumi baina ya Mataifa ya Afrika,
Caribbean na Pacific ili kuepusha vita, ambavyo kwa sasa vitakuwa ni vya
kiuchumi. Aidha, Rais huyo mstaafu ametaka muundo wa Baraza la Usalama
la Umoja wa Mataifa ufanyiwe marekebisho ili kuongeza nchi nyingine
ambazo zinastahili kuingia kwa sasa. Benjamin Mkapa amesisitiza kuwa,
kwa hali ilivyo sasa ni sababu za kiuchumi ndizo zinazoleta vita,
kutokana na uongozi mbaya, njaa na kiu ya baadhi ya nchi kutaka
maliasili za mataifa mengine. Mkapa amesema kama ninavyomnukuu:
“Hatutarajii kuwa na vita kama ile ya pili ya dunia, kwa sababu dunia
sasa inamiliki silaha kali kama za nyuklia, zinazoweza kuangamiza maisha
kwa wingi. Amesema ili kuzuia vita kutokea ndani ya nchi, ama kati ya
nchi mbili, ukanda, bara na hata dunia, kuna umuhimu wa serikali
zilizoko madarakani na hasa barani Afrika kuwekeza kwenye uongozi bora
na kuwashirikisha wananchi katika maamuzi ya kidemokrasia, yanayohusu
maisha na rasilimali za nchi zao
No comments:
Post a Comment