Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Thursday, 23 April 2015

“Waislamu wawatangazie walimwengu Uislamu halisi

Rais Hassan Rouhani amesema kulinda maisha na usalama wa watu, kutetea izza ya Ulimwengu wa Kiislamu na Umma wa Kiislamu na kuleta ustawi ni majukumu matatu muhimu waliyonayo Waislamu wote duniani. Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa wito huo jioni ya leo mjini Jakarta, Indonesia mbele ya hadhara ya maulama, wakuu, wasomi na shakhsia wa vyuo vikuu vya nchi hiyo na kusisitiza kwamba Waislamu wote wanapaswa kuvunja kimya chao mbele ya makundi ya kigaidi ambayo yameuhasiri vibaya zaidi Uislamu na kupaza sauti zao kwa pamoja kukabiliana na vitendo vya ukatili, kufurutu mipaka na ugaidi. Huku akisisitiza kuwa kuleta umoja katika Ulimwengu wa Kiislamu ndilo jukumu muhimu zaidi la Waislamu, Hujjatul Islam Rouhani amesema Uislamu ni dini ya wastani, mantiki na busara, na kwamba jukumu la Waislamu wote ni kuwabainishia walimwengu Uislamu halisi. Amesema leo hii kuna baadhi ya watu katika Ulimwengu wa Kiislamu ambao wameichafua izza ya Uislamu; na kwa kutumia jina la jihadi na dini wameinua panga kumuelekezea Mtume Mtukufu SAW; hivyo Waislamu wote wanapaswa wajihisi kuwa na jukumu la kukabiliana na hali hiyo. Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amebainisha kuwa Uislamu umeenea ulimwenguni kutokana na wito wake wa mantiki na upendo na kusisitiza kwamba Uislamu si dini ya upanga, bali ni dini ya mantiki, urehemevu, upendo na kuishi kwa amani na watu wengine na katu haumlazimishi mtu yeyote kuufuata…/

No comments:

Post a Comment