Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 13 April 2015

Kerry: Kongresi msiingilie mazungumzo ya nyuklia

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Marekani amewataka wajumbe wa kongresi ya nchi hiyo wasiingilie mazungumzo yanayoendelea ya nyuklia kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kundi la 5+1, kabla ya kumalizika muhula uliopangwa wa kumalizika mazungumzo hayo tarehe 30 Juni mwaka huu. Kwenye mahojiano aliyofanyiwa na Kanali ya Televisheni ya CBS ya Marekani, John Kerry amesema kuwa, kuanzia leo na kesho atatoa ufafanuzi kamili kwa wajumbe wa kongresi juu ya makubaliano yaliyofikiwa hivi karibuni huko Lausanne, Uswisi. Wakati huohuo, Rais Barack Obama  wa Marekani amesema kuwa, mizozo na mivutano  ya kichama na kimirengo  kuhusiana na kadhia ya nyuklia ya Iran yenye malengo ya amani na masuala mengine yanayohusiana na sera za kigeni za Washington inapaswa kusimamishwa. Rais Obama ameyasema hayo kwenye kikao cha kila mwaka cha wakuu wa nchi za bara la Amerika, kinachofanyika nchini Panama. Wiki iliyopita, Seneta John Sidney Mc Cain alisema kuwa, maelezo yaliyotolewa na viongozi wa Iran kuhusiana na makubaliano ya Lausanne ni sahihi zaidi na ya kimantiki zaidi, kuliko yale yaliyotolewa na  John Kerry Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Marekani. Hii ni katika hali ambayo, Maseneta wa mrengo wa Republican wanataka kukwamisha kufikiwa makubaliano ya mwisho, bila ya kuzingatia tahadhari iliyotolewa na serikali ya Obama ya kuwataka wajiepushe na uingiliaji wa mazungumzo hayo ya nyuklia. Maseneta hao wanashinikiza makubaliano ya mwisho ya nyuklia lazima yachunguzwe na kuangaliwa pia na wajumbe wa kongresi.

No comments:

Post a Comment