Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 20 April 2015

Daesh yachinja Wakristo 30 wa Ethiopia nchini Libya

Kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh limetoa mkanda wa video unaonyesha kundi hilo likiwachinja Wakristo wasiopungua 30 raia wa Ethiopia ambao walitekwa nyara na kundi hilo huko Libya. Mkanda huo wa video wa dakika 29 uliotolewa leo na kundi la kigaidi la Daesh unaonyesha magaidi wa Daesh wakiwauwa kwa kuwachinja raia wa Ethiopia wa dini ya Kikristo wasiopungua 12 katika pwani moja huko Libya na pia likiwapiga risasi kundi jingine la mateka 16 katika eneo la jangwani. Idadi kamili ya wahanga wa ukatili huo wa Daesh bado haijafahamika. Kundi la kigaidi la Daesh limeshaonyesha mikanda kadhaa ya video za ukatili na mauaji liliyoyafanya dhidi ya watu liliowateka nyara raia wa nchi mbalimbali kama Iraq, Syria, Marekani, Uingereza na Japan. Tarehe 15 mwezi huu mbunge mmoja wa Iraq ajulikanae kwa jina la Adel Khamis al Mahlawi alisema katika mkutano na vyombo vya habari kuwa, magaidi wa Daesh wamewauwa kwa kuwakata vichwa watu wasiopungua 300, ambao wengi wao wanaaminika ni kutoka makabila ya wanaohamahama katika mkoa wa al Anbar magharibi mwa Iraq

No comments:

Post a Comment