Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 13 April 2015

Ban Ki-Moon: Saudia acheni kuishambulia Yemen


Ban Ki moon Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametaka yaanzishwe mara moja mazungumzo ya kuleta amani nchini Yemen. Akihutubia kwenye mkutano wa kimataifa wa kukabiliana na jinai unaofanyika Doha, mji mkuu wa Qatar  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesisitiza juu ya kukomeshwa haraka mashambulizi ya kijeshi ya Saudi Arabia nchini Yemen sanjari na kuanzishwa mchakato wa mazungumzo ya kutafuta amani nchini humo. Ban Ki moon ameiambia Saudi Arabia na waitifaki wake kwenye machafuko ya Yemen kwamba, Umoja wa Mataifa uko tayari kuanzisha mchakato wa mazungumzo ya kutafuta amani nchini humo. Ban Ki moon amesisitiza kuwa, mazungumzo ya amani pekee ndiyo yatakayoweza kuutatua mgogoro wa Yemen. Takwimu zinaonyesha kuwa, wahanga wakuu wa mashambulio ya kijeshi ya Saudi Arabia na waitifaki wake nchini humo ni wanawake na watoto.

No comments:

Post a Comment