Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 27 April 2015

Al Marzouq: Malengo ya mapinduzi Tunisia hayajafikiwa

Rais wa zamani wa Tunisia amesema kuwa malengo ya Mapinduzi ya Januari 14 2011 hayajafikiwa nchini humo.Monsif al Marzouq Rais wa zamani wa Tunisia amesema kuwa tunapasa kukiri kuwa malengo na matakwa ya wananchi wa Tunisia kutokana na Mapinduzi ya mwezi Januari mwaka 2011 hayajafikiwa, kutokana na mapinduzi yaliyojiri dhidi ya mapambano hayo ya ukombozi. Al Marzouq ameashiria hali ya kiuchumi isiyoridhisha ya Tunisia kutokana na uchumi wa nchi kuwa tegemezi na kueleza kuwa, Tunisia imeshindwa kuboresha misingi ya kidemokrasia ya amani nchini na hadi sasa haijaweza kukomesha machafuko katika jamii kwa kuwaandalia wananchi  mazingira mazuri na salama.

No comments:

Post a Comment