Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 27 April 2015

Rais Putin: Marekani inawasaidia waasi wa Chechnya

Rais Vladmir Putin wa Russia ameituhumu Washington kuwa inatoa msaada wa kilojistiki wa  moja kwa moja kwa wanamgambo wa Qafqazi ya Kaskazini. Putin amesema Jumapili hii katika televisheni ya Rossiya 1 kuwa, vyombo vya kiitelijinsia vya Russia vimepata ushahidi unaoashiria msaada uliokuwa ukitolewa na Marekani kwa wanamgambo wa Qafqazi ya Kaskazini mwanzoni mwa mwaka 2000.  Rais Vladmir Putin wa Russia amebainisha hayo Jumapili hii katika filamu iliyopewa jina la "Rais" kwa mnasaba wa kuadhimisha miaka 15 tangu awe Rais wa nchi kwa mara ya kwanza.  Rais Putin amesema  alimtaarifu Rais wa Marekani wa wakati huo kuhusu hatua za uingiliaji kati za Washington, na kisha Rais wa Marekani alimjibu kwa kusema, atasitisha misaada ya nchi yake kwa waasi hao wa Qafqazi ya Kaskazini. Hata hivyo baada ya siku 10,  wakuu wa shirika la ujasusi la Russia FSB walipokea barua kutoka kwa wenzao wa Washington wakisema kuwa, wamekuwa na wataendelea kuwa na  mahusiano na makundi ya upinzani ya Russia; na kwamba wanaona wana haki ya kufanya hivyo, na wataendelea kufanya hivyo hata katika siku za usoni.

No comments:

Post a Comment