Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Thursday, 23 April 2015

Mawaziri wa Ulinzi wa Afrika Mashariki wakutana Sudan

Mawaziri wa Ulinzi wa nchi kadhaa za Afrika Mashariki wanakutana Khartoum mji mkuu wa Sudan katika mkutano wa siku tatu wenye lengo la kujadili changamoto za kiusalama. Mawaziri wa Ulinzi wa Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia, Djibouti, Visiwa vya Comoro, Sudan Kusini, Ushelisheli na mwenyeji Sudan wanashiriki katika mkutano huo ulioanza jana. Akihutubia katika kikao cha ufunguzi wa mkutano huo, Abdul Rahim Muhammad Hussein, Waziri wa Ulinzi wa Sudan amesema kuwa, ni jambo la dharura kwa nchi za Afrika Mashariki kufanya kila ziwezalo kukabiliana na changamoto za kiusalama zinazozikabili. Amesema kuwa, kuna haja ya kutumiwa suhula na mikakati yote kwa ajili ya kukabiliana na migogoro ili kuhakikisha amani na uthabiti vinatawala barani Afrika. Aidha Waziri wa Ulinzi wa Sudan amesisitiza juu ya kuweko uratibu wa juhudi kwa lengo la kuhitimisha migogoro, mivutano na mapigano sambamba na kupunguza machungu ya watu kupitia ufumbuzi wa kisiasa, kiusalama na ustawi wa mwanadamu. Waziri wa Ulinzi wa Sudan ametoa wito pia wa kuimarishwa sekta ya ulinzi kwa nchi za Kiafrika kwa kutumiwa vyema vyanzo vya utajiri na uwezo wa nguvu kazi ya bara la Afrika

No comments:

Post a Comment