Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 13 April 2015

Abiria 18 wateketea kwa moto katika ajali Tanzania



Watu 18 wameteketea kwa moto katika ajali ya barabarani nchini Tanzania baada ya basi la Kampuni ya Nganga Express na lori aina ya Fuso kugongana uso kwa uso na kuwaka moto katika eneo la Iyovi, Milima ya Uduzungwa, mkoani Morogoro. Katika ajali hiyo iliyotokea abiria 15 waliokuwa kwenye basi na wengine watatu wa lori waliteketea kwa moto huku wengine 10 wakijeruhiwa vibaya.  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leonard Paul amesema  kuwa, ajali hiyo ilitokea baada basi hilo lililokuwa linatoka Kilombero kwenda Mbeya likiwa kwenye mistari ya barabarani ya katazo na kwenye mwendo kasi kugongana na lori lililokuwa limebeba matikiti na kuwaka moto. Alisema majeruhi wanne wamelazwa katika Hospitali ya St. Kizito, Mikumi na sita wako katika Hospitali ya Mtandika, Iringa.  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro ameongeza kuwa,  kwenye basi hilo kulikuwa na pikipiki ambayo pia iliungua inawezekana ndiyo iliyosababisha moto huo. Ajali hiyo ni mfululizo wa ajali zinazotokea katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania juma hili, ikiwa ni siku moja baada ya watu watano kufariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa katika mikoa ya Dodoma na Iringa. Tanzania imekuwa ikishuhudia ajali za mara kwa mara za barabarani ambapo  makumi ya watu wamekuwa wakipoteza maisha yao. Uzembe wa madereva na mwendo wa kasi zinatajwa kuwa sababu kuu zinazosababisha mlolongo wa ajali nchini Tanzania.

No comments:

Post a Comment