Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Wednesday, 29 April 2015

Iran na Syria: Magaidi waangamizwe Syria

Mawaziri wa Ulinzi wa Iran na Syria wamesisitiza juu ya udharura wa kudumishwa mapambano ya pande zote dhidi ya ugaidi.
Waziri wa Ulinzi wa Iran Brigedia Jenerali Hussein Dehqan amesema vita vya kulazimishwa vya matakfiri na Uzayuni dhidi ya wananchi wa Syria  ni vita vinavyopiganwa kwa niaba ya upande mwingine na stratejia ya pamoja ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel. Brigedia Jenerali Dehqan amesema kuwa lengo la vita hivyo ni kuudhaminia usalama wa kudumu utawala wa Kizayuni, kuzidhoofisha na kuzigawa nchi za Kiislamu, kubadili muundo wa eneo la Mashariki ya Kati, kukabiliana na wimbi la mwamko wa Kiislamu na mwishowe kulidhibiti kikamilifu eneo la Mashariki ya Kati.
Waziri wa Ulinzi wa Iran ameyasema hayo leo hapa Tehran katika mazungumzo yake na Fahd Jasim al Furayj, Waziri wa Ulinzi wa Syria aliyeko ziarani nchini Iran.
Brigedia Jenerali Hussein Dehqan amepongeza muqawama na mapambano ya wananchi na vikosi shupavu vya jeshi la Syria dhidi ya magaidi na vibaraka kutoka nchi mbalimbali duniani na kuongeza kuwa: Kuendelezwa muqawama huo kusambaratishaa makundi ya kitakfiri na kigaidi.
Kwa upande wake Waziri wa Ulinzi wa Syria Meja Jenerali Fahd Jassem al-Freij amewapongeza wananchi na serikali ya Iran kwa kuwaunga mkono wananchi na serikali ya Syria katika mapambano yao dhidi ya magaidi na kueleza kuwa: Wananchi wa Syria kamwe hawatasahau msaada na uungaji mkono wa wananchi na serikali ya Iran. Waziri wa Ulinzi wa Syria amesema kuwa Iran ya Kiislamu ni mhimili na msingi mkuu wa mapambano na kuongeza kuwa, ushindi huu mkubwa usingepatikana iwapo kusingekuwepo uungaji mkono wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran

No comments:

Post a Comment